Jinsi ya kutengeneza Sambusa

 

somali sambusa 001

Mahitaji

  • Nyama ya kusaga 1kg
  • Viungo (2tsp turmeric, 1 tbsp ginger powder, 2tbsp paprika powder, 2tbsp curry powder, 2tbsp meat flavour stock)
  • Vitunguu 2-3 vikubwa
  • Hoho 1
  • Thomu iliyosagwa 2tbsp
  • Carrot zilizokwanguliwa 250mg (grated carrots)
  • Manda za sambusa (spring roll pastry)
  • Mafuta ya kukaangia
  • parsley/coriander (dania)
  • Limau 2-3
  • Ngano ya kufungia manda

Jinsi ya kutengeneza

  • Weka mchanyiko wa nyama, viungo, thomu, juice ya limau  kwenye sufuria kubwa. Kisha bandika jikoni.
  • Kataka vitunguu, dania na hoho vipande vidogovidogo na vyembamba. Kisha visafishe, bila kusahau carrot zako. Zichuje vizuri.
  • Usisahau kuigeuza nyama yako. Onja km imeiva
  • Mimina mchanganyiko wa vitunguu kwenye nyama. Acha ichemke kwa dakika 5-10, kisha onja kama chumvi na viungo vipo sawa. Kama ndogo ongeza. kisha acha ichemke mpaka ukavu maji. Hakikisha imekauka. Kisha zima jiko. Acha ipoe
  • Weka ngano kwenye kibakuli, weka maji, koroga ilikupata mchanganyiko *gundi*
  • Funga manda zako, jaza sambusa. Bonyeza link hapo chini kama hujui jinsi ya kufunga sambusa.
  • Linka ya YouTube —   https://www.youtube.com/watch?v=TR9F993TiM4
  • Choma sambusa zako. Tayari Kula.
  • Unaweza kuchoma zote au ukahifadhi baadhi kwenye freezer.

 

PhotoGrid_1553258217971Baadhi ya spices nlizotumia mie. Unaweza tumia unazopenda weye mwenyewe.

PhotoGrid_1553260242844Carrot unaweza nunua zima, kisha ukazikwangua mwenyewe nyumbani. Mie nanunuaga zilizo kwanguliwa tayari.

PhotoGrid_1553258292669Pia unaweza tumia nyama ya kusanga ya kuku, binafsi napenda sambusa za nyama ya kusaga ya ng’ombe.

20181121_161519

Unaweza kutengeneza manda zako mwenyewe.

PhotoGrid_1553258174557Kuna wanaotumia mayai badala ya ngano kufungia sambusa zao.

20190322_14590220190322_14584920190322_145924