Jinsi ya kutengeneza ndizi za mzuzu na nazi ya kupaka

Asalaam aleikum warahmatullah wabarakatu, natumai swaum zinaendelea salama. Safari hii nimechelewa kupost mapishi ya iftar, kuna baadhi ya mapishi nataka nijaribu, nikiyapatia vizuri In shaa Allah nizipost. Ila kwa sasa hivi ntapost marudio ya mapishi ya ramadhani ya mwaka jana.

Mwenyezimungu abariki funga zetu na apokee swaum zetu. Ramadhan njema.

Mahitaji

  • Ndizi mzuzu kilo moja
  • Nazi 400ml
  • Maji 400ml
  • Iliki

Maandalizi

  • Menya, kata ndizi zako
  • Weka ndizi, nazi 200ml, maji 400ml na iliki kwenye sufuria, kisha bandika jikoni viive.
  • Angalia zisiive sana kiasi cha kumong’onyoka. Zikisha iva, zima jiko.

Jinsi ya kutengeneza tui la kupaka

Mahitaji

  • Nazi 200ml
  • Ngano kijiko kidogo nusu (hii unatumia kama tui lako ni jepesi mno)


Maandalizi

  • Chemsha tui lako kwenye kisufuria kidogo. Likianza kuchemka, koroga taratibu hadi liive ili tui lisikatike.
  • Tui lako litakuwa tayari kama likiwa zito na linatoa mapovu wakati likichemka.
  • Ikiwa tui lako ni jepesi na haliwi zito, changanya ngano na maji vijiko vikubwa vitatu, kisha mimina taratibu kwenye tui lako. Usimimine lote kwa wakati mmoja, likianza kuwa zito, acha lichemke mpk liive.
  • Changanya tui lako na ndizi kwa kutumia kijiko. Fanya hivi taratibu kuepusha ndizi kumong’onyoka.
  • Ndizi zako tayari kwa kuliwa.

Jinsi ya kutengeneza sambusa

Mahitaji

  • Nyama ya kusaga 1kg
  • Viungo (2tsp turmeric, 1 tbsp ginger powder, 2tbsp paprika powder, 2tbsp curry powder, 2tbsp meat flavour stock)
  • Vitunguu 2-3 vikubwa
  • Hoho 1
  • Thomu iliyosagwa 2tbsp
  • Carrot zilizokwanguliwa 250mg (grated carrots)
  • Manda za sambusa (spring roll pastry)
  • Mafuta ya kukaangia
  • parsley/coriander (dania)
  • Limau 2-3
  • Ngano ya kufungia manda

Jinsi ya kutengeneza

  • Weka mchanyiko wa nyama, viungo, thomu, juice ya limau  kwenye sufuria kubwa. Kisha bandika jikoni.
  • Kataka vitunguu, dania na hoho vipande vidogovidogo na vyembamba. Kisha visafishe, bila kusahau carrot zako. Zichuje vizuri.
  • Usisahau kuigeuza nyama yako. Onja kama imeiva
  • Mimina mchanganyiko wa vitunguu kwenye nyama. Acha ichemke kwa dakika 5-10, kisha onja kama chumvi na viungo vipo sawa. Kama ndogo ongeza. kisha acha ichemke mpaka ukavu maji. Hakikisha imekauka. Kisha zima jiko. Acha ipoe
  • Weka ngano kwenye kibakuli, weka maji, koroga ilikupata mchanganyiko *gundi*
  • Funga manda zako, jaza sambusa. Bonyeza link hapo chini kama hujui jinsi ya kufunga sambusa.
  • Choma sambusa zako. Tayari Kula.
  • Unaweza kuchoma zote au ukahifadhi baadhi kwenye freezer.

How to fold Samosa (2 Ways) By Rubina Asif – YouTube

Jinsi ya kutengeneza mahamri

Mahitaji

  • Ngano 1kg
  • Sukari robo (kama weye ni mpenzi wa sukari, unaweza ukaongeza)
  • Hamira packet 2 za 7g
  • Bakingpowder paket 1 ya 7g
  • Nazi au maziwa 1ltr
  • Iliki iiyosagwa 2tbs
  • Mayai 3
  • Mafuta ya kupikia 1ltr
  • Makuli kubwa la kukandia
  • Karai
  • Kibao na msukumio

Maandalizi

  • Mimina mafuta kidogo au samli (150ml) kwenye kisufuria kidogo, kisha iweke jikoni yapate moto.
  • Mimina unga, sukari na iliki kwenye bakuli la kukandia, kisha vichanganye vizuri
  • Mafuta yakishapata moto vizuri mimina kwenye mcchanganyiko wa unga, angalia usiungue.
  • Changanya mafuta na unga vizuri, kisha weka hamira na bakingpowder. Changanya vizuri
  • Vunja mayai na changanya kwenye mchanganyiko wa unga.
  • Mimina nazi au maziwa ya uvuguuvugu taratibu kwenye unga, mpaka upate donge moja. Mchanganyiko usiwe mgumu sana na usiwe chapachapa.
  • Kanda ngano yako hadi iumuke.
  • Kata madonge tisa. Sukuma kisha kata.
  • Bandika Karai lako, weka mafuta, anza kuchoma mahamri yako.
  • Yakiwa rangi ya brown, yatoe.
  • Mahamri yako tayari kuliwa.

Unaweza kula na mbaazi, maharage au mchuzi.