Jinsi ya kutengeneza mahamri

Mahitaji

  • Ngano 1kg
  • Sukari robo (kama weye ni mpenzi wa sukari, unaweza ukaongeza)
  • Hamira packet 2 za 7g
  • Bakingpowder paket 1 ya 7g
  • Nazi au maziwa 1ltr
  • Iliki iiyosagwa 2tbs
  • Mayai 3
  • Mafuta ya kupikia 1ltr
  • Makuli kubwa la kukandia
  • Karai
  • Kibao na msukumio

Maandalizi

  • Mimina mafuta kidogo au samli (150ml) kwenye kisufuria kidogo, kisha iweke jikoni yapate moto.
  • Mimina unga, sukari na iliki kwenye bakuli la kukandia, kisha vichanganye vizuri
  • Mafuta yakishapata moto vizuri mimina kwenye mcchanganyiko wa unga, angalia usiungue.
  • Changanya mafuta na unga vizuri, kisha weka hamira na bakingpowder. Changanya vizuri
  • Vunja mayai na changanya kwenye mchanganyiko wa unga.
  • Mimina nazi au maziwa ya uvuguuvugu taratibu kwenye unga, mpaka upate donge moja. Mchanganyiko usiwe mgumu sana na usiwe chapachapa.
  • Kanda ngano yako hadi iumuke.
  • Kata madonge tisa. Sukuma kisha kata.
  • Bandika Karai lako, weka mafuta, anza kuchoma mahamri yako.
  • Yakiwa rangi ya brown, yatoe.
  • Mahamri yako tayari kuliwa.

Unaweza kula na mbaazi, maharage au mchuzi.

Leave a Reply

Please log in using one of these methods to post your comment:

WordPress.com Logo

You are commenting using your WordPress.com account. Log Out /  Change )

Facebook photo

You are commenting using your Facebook account. Log Out /  Change )

Connecting to %s