Jinsi ya kutengeneza vitumbua

Mahitaji

  • Mchele vikombe viwili (nusu kilo) loweka usiku kucha
  • Tui vikombe viwili
  • Sukari kikombe kimoja
  • Hamira packet moja (kijiko kimoja)
  • Iliki kijiko kimoja cha chai
  • Mayai mawili
  • Mafuta ya kupikia

Maandalizi

  • Kikombe utakachotumia kupimia mchele, ndicho utakachopimia sukari na tui.
  • Chuja mchele uloloweka vizuri, hakikisha hamna maji yamebakia
  • Mimina tui, mchele, sukari, iliki na hamira kwenye blender, chanya mchanganyiki kwa kutumia kijiko ili iwe sawa kisha washa blender lako.
  • Saga kwa takriban dakika 10, pumzisha blender lako kila baada ya dakika 2- 3 hii ni kuepusha blender lako lisiungue. Saga hadi uwe laini.
  • Angalia uzito ulivyo, kama mzito sana ongeza tui kidogo.
  • Weka mchanganyiko wako kwenye bakuli, ufunike na kisha uweke kwenye sehemu yenye joto uumuke . Unaweza uacha uumuke kwa lisaa limoja au mawili au ukiuona ujazo umekuwa marambili yake.
  • Baada ya kuumuka weka mayai mawili, kisha changanya mchanganyiko wako vizuri kwa kutumia upawa.
  • Bandika kikaangio chako cha vitumbua jikoni na mchanganyiko upo tayari kwa kuchoma.

Enjoy!!!!!

Jinsi ya kutengeneza chapati za maji za hoho

Ftari yetu ya leo tunatengeneza chapati za maji za hoho. Chapati zetu zitakuwa za chumvi maana ftari kuu zengine zote nazo ni za chumvi, kwahiyo na chapati zetu tutaweka chumvi. Ila kama unaweza kuchanganya chumvi na sukari, unaweza ukaweka sukari badala ya chumvi, ila hoho sikushauri kuweka kwenye chapati za maji za sukari, utaharibu ladha.

Mahitaji

  • Ngano nusu kilo
  • Maziwa 300ml
  • Maji 200ml
  • Hoho nusu
  • Chumvi kijiko kidogo nusu
  • Mafuta ya kukaangia

Jinsi ya kupika

  • Osha hoho, kisha ikate vipande vidogovidogo
  • Changanya vitu vyote, kama mchanganyiko mzito sana ongeza maji kidogo.
  • Kaanga chapati zako.

Jinsi ya kutengeneza ndizi za mzuzu na nazi ya kupaka

Asalaam aleikum warahmatullah wabarakatu, natumai swaum zinaendelea salama. Safari hii nimechelewa kupost mapishi ya iftar, kuna baadhi ya mapishi nataka nijaribu, nikiyapatia vizuri In shaa Allah nizipost. Ila kwa sasa hivi ntapost marudio ya mapishi ya ramadhani ya mwaka jana.

Mwenyezimungu abariki funga zetu na apokee swaum zetu. Ramadhan njema.

Mahitaji

  • Ndizi mzuzu kilo moja
  • Nazi 400ml
  • Maji 400ml
  • Iliki

Maandalizi

  • Menya, kata ndizi zako
  • Weka ndizi, nazi 200ml, maji 400ml na iliki kwenye sufuria, kisha bandika jikoni viive.
  • Angalia zisiive sana kiasi cha kumong’onyoka. Zikisha iva, zima jiko.

Jinsi ya kutengeneza tui la kupaka

Mahitaji

  • Nazi 200ml
  • Ngano kijiko kidogo nusu (hii unatumia kama tui lako ni jepesi mno)


Maandalizi

  • Chemsha tui lako kwenye kisufuria kidogo. Likianza kuchemka, koroga taratibu hadi liive ili tui lisikatike.
  • Tui lako litakuwa tayari kama likiwa zito na linatoa mapovu wakati likichemka.
  • Ikiwa tui lako ni jepesi na haliwi zito, changanya ngano na maji vijiko vikubwa vitatu, kisha mimina taratibu kwenye tui lako. Usimimine lote kwa wakati mmoja, likianza kuwa zito, acha lichemke mpk liive.
  • Changanya tui lako na ndizi kwa kutumia kijiko. Fanya hivi taratibu kuepusha ndizi kumong’onyoka.
  • Ndizi zako tayari kwa kuliwa.

How To Make Sambusa

somali sambusa 001

After many requests, here is the english version of “how to make sambusa” for those who dont understand Swahili. Enjoy!!!

Ingredients
– Minced beef 1kg
– Spring roll sheets (spring roll pastry) – you can buy them at the African shops, Chinese supermarket).
– Spices (2tsp of tumeric powder, 2tbsp of paprika powder, 1tbsp of ginger powder, 2-3 tbsp of curry powder, 2-3 tbsp of beef flavour broth): I love spices (I never measure) + I do not use salt 😊
– 2tbsp Garlic paste
– 2 large onions: cut into small thin pieces
– 1 bell pepper: same
– Half bag of grated carrots
– 2-3 lemons: squeeze
– Frying oil
– Flour for folding
– Coriander / parsley

Lets do this 😉
– Remove the spring roll sheets from the freezer on time (I usually take them out the night before and put them in the fridge. Then they will be defrosted the next day).
– Put the minced meat, herbs, lemon juice + garlic in a large pan. Bring this to boil
– Meanwhile, cut the onions, bell pepper and coriander / parsley.
– Clean the pieces of onions, peppers, carrots and coriander / parsley.
– Don’t forget your minced meat, stir occasionally.
– When the minced meat is cooked, put the onions + bell pepper + carrots + coriander / parsley, stir well … and let it cook for 5-8 minutes.
– Taste whether there is enough seasoning / salt. If not, add a little. I usually add cubes of broth and curry powder.
– Let the meat boil, must be dry, otherwise they will leak.
– If the meat is cooked and well, turn off the fire. Let it cool off.
– Put 5-6 scoops of flour in a bowl and add water. Stir well, it should not be too thick or thin. This is your “glue”.
– Next step = folding  YouTube link. It is a bit difficult to explain Hahaha

– Fold, fill with minced meat & fold up.
– Fry your sambusa…… Ready to eat. Enjoy 😉

Ps: You dont have to fry them all, you can keep them in the freezer.

PhotoGrid_1553258217971

These are the spices I used.

I make my own garlic paste. You can grate the carrots yourself, but I prefer buying the ones that are already done.

PhotoGrid_1553258174557

Some people use eggs for folding. I use flour.

Jinsi ya kutengeneza Sambusa

 

somali sambusa 001

Mahitaji

  • Nyama ya kusaga 1kg
  • Viungo (2tsp turmeric, 1 tbsp ginger powder, 2tbsp paprika powder, 2tbsp curry powder, 2tbsp meat flavour stock)
  • Vitunguu 2-3 vikubwa
  • Hoho 1
  • Thomu iliyosagwa 2tbsp
  • Carrot zilizokwanguliwa 250mg (grated carrots)
  • Manda za sambusa (spring roll pastry)
  • Mafuta ya kukaangia
  • parsley/coriander (dania)
  • Limau 2-3
  • Ngano ya kufungia manda

Jinsi ya kutengeneza

  • Weka mchanyiko wa nyama, viungo, thomu, juice ya limau  kwenye sufuria kubwa. Kisha bandika jikoni.
  • Kataka vitunguu, dania na hoho vipande vidogovidogo na vyembamba. Kisha visafishe, bila kusahau carrot zako. Zichuje vizuri.
  • Usisahau kuigeuza nyama yako. Onja km imeiva
  • Mimina mchanganyiko wa vitunguu kwenye nyama. Acha ichemke kwa dakika 5-10, kisha onja kama chumvi na viungo vipo sawa. Kama ndogo ongeza. kisha acha ichemke mpaka ukavu maji. Hakikisha imekauka. Kisha zima jiko. Acha ipoe
  • Weka ngano kwenye kibakuli, weka maji, koroga ilikupata mchanganyiko *gundi*
  • Funga manda zako, jaza sambusa. Bonyeza link hapo chini kama hujui jinsi ya kufunga sambusa.
  • Linka ya YouTube —   https://www.youtube.com/watch?v=TR9F993TiM4
  • Choma sambusa zako. Tayari Kula.
  • Unaweza kuchoma zote au ukahifadhi baadhi kwenye freezer.

 

PhotoGrid_1553258217971Baadhi ya spices nlizotumia mie. Unaweza tumia unazopenda weye mwenyewe.

PhotoGrid_1553260242844Carrot unaweza nunua zima, kisha ukazikwangua mwenyewe nyumbani. Mie nanunuaga zilizo kwanguliwa tayari.

PhotoGrid_1553258292669Pia unaweza tumia nyama ya kusanga ya kuku, binafsi napenda sambusa za nyama ya kusaga ya ng’ombe.

20181121_161519

Unaweza kutengeneza manda zako mwenyewe.

PhotoGrid_1553258174557Kuna wanaotumia mayai badala ya ngano kufungia sambusa zao.

20190322_14590220190322_14584920190322_145924

Wali wa carrot na kuku wakukaanga

Vipimo Vya Wali
– Mchele wa Basmati/Pishori – 1 kilo moja
– Vitunguu maji – 3
– Karoti – 2
– Siagi – 3 vijiko vya supu
– Kidonge cha supu (stock) – 1 kimoja
– -Chumvi – kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
– Osha mchele uroweke kama saa moja au mbili
– Katakata vitunguu vipande vidogodogo (chopped) weka kando.
– Kwaruza karoti (grate) weka kando.
– Tia siagi katika sufuria ya kupikia wali, weka katika moto iyayuke
– Kaanga vitunguu hadi vigeuke rangi kiasi tu.
– Tia maji kiasi ya kupikia wali, changanya na kidonge cha supu.
– Yakichemka tia mchele, koroga, funika uweke moto mdogo mdogo.
– Kabla ya maji kukauka tia karoti changanya wali kisha funika uive kama unavyopika pilau.

Vipimo Vya Kuku Wa Kukaanga
– Kuku alokatwakatwa – 1
– Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi ilosagwa – 2 vijiko vya supu
– Bizari ya mchanganyiko/garam masala – kijiko cha supu
– Mtindi/Yoghurt – 1 kijiko cha supu
– Ndimu – 1
– Chumvi – kiasi
– Mafuta ya kukaangia – kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
– Ukishamuosha kuku, mchuje atoke maji yote.
– Changanya viungo vyote katika kibakuli kidogo.
– Changanya pamoja na kuku kisha acha akolee viungo (marinate) kwa muda wa masaa  mawili takriban.
– Weka mafuta katika karai na kaanga kuku, akiwiva yu tayari kuliwa na wali.

Jinsi ya kutengeneza Mahamri

Gerelateerde afbeelding

Mahitaji

  • Ngano 1kg
  • Sukari robo (kama weye ni mpenzi wa sukari, unaweza ukaongeza)
  • Hamira packet 2 za 7g
  • Bakingpowder paket 1 ya 7g
  • Nazi au maziwa 1ltr
  • Iliki iiyosagwa 2tbs
  • Mayai 3
  • Mafuta ya kupikia 1ltr
  • Makuli kubwa la kukandia
  • Karai
  • Kibao na msukumio

 

Maandalizi

  • Mimina mafuta kidogo au samli (150ml) kwenye kisufuria kidogo, kisha iweke jikoni yapate moto.
  • Mimina unga, sukari na iliki kwenye bakuli la kukandia, kisha vichanganye vizuri
  • Mafuta yakishapata moto vizuri mimina kwenye mcchanganyiko wa unga, angalia usiungue.
  • Changanya mafuta na unga vizuri, kisha weka hamira na bakingpowder. Changanya vizuri
  • Vunja mayai na changanya kwenye mchanganyiko wa unga.
  • Mimina nazi au maziwa ya uvuguuvugu taratibu kwenye unga, mpaka upate donge moja. Mchanganyiko usiwe mgumu sana na usiwe chapachapa.
  • Kanda ngano yako hadi iumuke.
  • Kata madonge tisa. Sukuma kisha kata.
  • Bandika Karai lako, weka mafuta, anza kuchoma mahamri yako.
  • Yakiwa rangi ya brown, yatoe.
  • Mahamri yako tayari kuliwa.

Unaweza kula na mbaazi au mchuzi.